Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_6eb0189da76744c078d5d9e089fd0dbf, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_fff88ee855c99b199163a8fa8e97c11f, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/right_sidebar.php on line 13

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/right_sidebar.php on line 13
Sidebar with Floating Button
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_03837d6b73a06a961848f8536c50f8ae, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 3

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 3

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_033875989a8233d0b2eaefc498ebb148, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 14

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/top_menu.php on line 14
MHUBIRI
☰
AckyShine
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_922f07e9bac4770a38c052763549571e, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line 4

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

Featured Image

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.// Waniangalia sana,/ siyo kwa kunipeleleza,/ lakini kwa sababu wapenda kuniona hivi karibu na wewe,/ wafurahiwa nikija kukuabudu./ Wayasikiliza maneno yangu yote/ yenye kutoka mdomoni mwangu,/ na zaidi wapokea maneno yangu yanayotoka moyoni./ Nataka kuzungumza na wewe peke yako,/ na kusahau mambo mengine yote/ na watu wengine walioko kanisani pamoja nami./

Yesu wangu,/ nakushukuru/ kwa sababu umekubali kutupa Sakramenti hii kuu kabisa,/ ukitaka kukaa pamoja na sisi,/ na hata ukakubali kuwa chakula chetu/ chenye nguvu ya ajabu./ Mfalme wangu Yesu,/ Sultani wangu Mkuu,/ naamini kabisa kwamba upo katika Altare/ na kwamba umejificha chini ya umbo la mkate./ Ulipokuwapo bado hapa duniani mbele za watu,/ ulikuwa hujifichi kama sasa;/ lakini hata siku zile/ watu hawakuweza kukuona vile ulivyo./ Hawakuweza kuutambua Umungu wako,/ ikalazimu kukuamini tu sawa kama sisi./ Wakainama kichwa wakisema,/ β€œBwana wangu na Mungu wangu”./ Na mimi kadhalika naungama/ U Bwana wangu na Mungu wangu/ na Mkombozi wangu/ na salama yangu yote./ U Yesu wangu tu,/ siwezi kusema zaidi./ Nakuabudu ee Yesu./ Najua sana, mimi ni mdogo kabisa,/ sina maana hata kidogo./ Mimi ni dhaifu na maskini mno./ Lakini Wewe katika hruuma yako kubwa/ waniita nije kwako./ Wewe huuangalii umaskini wangu,/ bali wanivuta katika mapendo yako./

Nasikia maneno yako usemayo:/ β€œNjooni kwangu ninyi nyote mnaoelemewa na mizigo/ nami nitawasaidia”./ Kwa ajili ya maneno hayo/ nakuja kwako bila hofu./ Najua kwamba wanipenda,/ najua wataka kunisaidia na kuniponya,/ najua kuwa wataka kunitakasa./

Nahitaji sana msaada wako, hakika./ Unaniona katika mwendo wangu wa kila siku,/ Jinsi ninavyohangaika na vishawishi mara nyingi;/ jinsi nilivyo na lazima ya kushindana kila siku/ nikitaka kukaa mwema na safi katika utumishi wako./ Naungama mbele yako Wewe Mkombozi wangu,/ kwamba sikukaa imara siku zote vile nilivyopaswa./ Naungama kwamba nimeshindwa mara nyingine/ na kwa hivi naomba toba./ Lakini kwa nini nimeshindwa mara nyingine?/ Kwa nini nikakosa?/ Ni kwa sababu nalikuwa nimekwenda mbali nawe;/ nalianza kujitegemea mwenyewe./ Katika majivuno yangu nikajisifu mwenyewe,/ nikajiona mwema,/ nikasahau udhaifu wangu./ Na kwa ajili hiyo nikajitia katika hatari bure,/ sikujilinda tena,/ nikampa shetani nafasi ya kunishambulia kwa hila zake zote./ Unihurumie ee Yesu wangu./

Sasa nafahamu jinsi nilivyokuwa mjinga kwelikweli./ Ndiyo maana nakuabudu kwa moyo wangu wote./ Najiweka mikononi mwako/ ufanye nami vile unavyotaka./ Wewe utanitunza;/ Wewe utanilinda vema;/ Wewe utaniongoza nijue namna ya kuepa hatari zote,/ na jinsi ya kufukuza kila kishawishi./ Chukua moyo wangu kabisa,/ kwa sababu ni mali yako kamili;/ Wewe ndiwe uliyeniumba,/ ndiwe uliyenipeleka katika Ukristo,/ nawe ndiwe utakayenihukumu siku ya mbele./ Ndivyo ninavyojitolea kwako./ Ndivyo ninavyokuabudu,/ wala sijui njia nyingine ya kukusifu zaidi./

Yesu wangu mpenzi,/ naomba upokee kwa uzuri heshima hiyo yangu./ Angalia: naitolea pamoja na heshima yote/ unayopewa daima na watakatifu wako/ na malaika wako./ Nikipiga magoti hapa mbele yako sasa,/ siko peke yangu,/ nakuabudu pamoja na Mama yako Bikira Maria,/ ambaye sala zake zinakupendeza kabisa./ Sala zangu naweka pamoja na sala zake yeye,/ uzipokee zote pamoja,/ zikupendeze zote sawa./ Ee Mama Maria!/ Nifundishe maneno ya kumsifu Mwanao Yesu vizuri./ Nipeleke kwa Yesu tumwabudu pamoja./ Nifunike na utakatifu wako/ kusudi Yesu asiangalie tena umaskini wangu/ na makosa yangu,/ aniponye katika huruma yake./

Sasa najisikia vizuri, Yesu wangu./ Sasa nina moyo wa kuweza kuendelea vema/ katika njia njema./ Sasa ninatumaini kwamba/ nitakaa mkristo mwema,/ nitakuwa mtumishi wako mwaminifu./ Nasikia amani kubwa sana moyoni mwangu,/ kwa kuwa nimo mikononi mwako./ Baada ya dakika chache/ nitaondoka tena kanisani,/ nitarudi nyumbani kwangu,/ lakini hatutaachana,/ hapana./ Mapendo yetu yatatuunganisha pamoja daima./ Wewe utanikumbuka nikiwa kazini,/ nikilala usingizi,/ nikienda njiani,/ kila mahali nilipo,/ Wewe utaniona,/ utafuatana na mimi./ Kadhalika nitakukumbuka tu./ Nitafanya bidii nisikuache kabisa./ Amina.

AckySHINE Solutions

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_5c097c6cb7e9c7a81fd381b969fb50c9, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line 4

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Raphael Okoth (Guest) on August 1, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Elizabeth Mrope (Guest) on June 18, 2017

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Andrew Mahiga (Guest) on April 24, 2017

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Charles Mboje (Guest) on April 18, 2017

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Esther Nyambura (Guest) on April 2, 2017

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Kevin Maina (Guest) on April 1, 2017

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Victor Sokoine (Guest) on February 27, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Andrew Mchome (Guest) on February 24, 2017

Mungu akubariki!

Grace Mligo (Guest) on November 19, 2016

Sifa kwa Bwana!

Grace Mushi (Guest) on November 3, 2016

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Betty Kimaro (Guest) on August 8, 2016

Mwamini Bwana; anajua njia

Mercy Atieno (Guest) on July 16, 2016

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Benjamin Masanja (Guest) on June 16, 2016

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Edward Chepkoech (Guest) on June 16, 2016

Mungu ni mwema, wakati wote!

Francis Mtangi (Guest) on June 7, 2016

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

George Ndungu (Guest) on April 17, 2016

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

John Kamande (Guest) on March 23, 2016

Neema na amani iwe nawe.

Robert Ndunguru (Guest) on November 15, 2015

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Bernard Oduor (Guest) on November 15, 2015

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Betty Akinyi (Guest) on October 31, 2015

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Catherine Mkumbo (Guest) on October 11, 2015

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Violet Mumo (Guest) on June 22, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Lucy Kimotho (Guest) on June 3, 2015

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Related Posts

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkinga... Read More

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yes... Read More

Malkia wa Mbingu

Malkia wa Mbingu

Malkia wa mbingu, furahi, aleluya. Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya. Amefufuka alivyosema, A... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuhesh... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Kwa jina la Baba….. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,M... Read More
SALAMU MARIA

SALAMU MARIA

Salamu Maria
Umejaa neema
Bwana yu nawe
Umebarikiwa kuliko wanawake wote
Na Y... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More


Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_db537ceb037685c09adcd7c94ae53278, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/mhubiri/bottom_menu.php on line 3

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/mhubiri/bottom_menu.php on line 3