Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_461e8c9950d3c5ad7218fca1a3e1847a, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Je, kwa nini akina mama wajawazito hawatakiwi kunywa pombe?
Date: April 15, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Wanawake wajawazito ambao hunywa pombe au kuvuta sigara
wanahatarisha afya na maisha ya mtoto aliye tumboni. Mtoto aliye
tumboni hurutubishwa kupitia damu ya mama. Kama mama atavuta
sigara au kunywa pombe, sumu illiyopo katika sigara au pombe
inapoingia kwenye damu yake itamfikia mtoto pia. Pombe hushambulia
moyo uendeleao kukua na ubongo wa mtoto aliye tumboni.
Akina mama wanaokunywa kupita kiasi wakiwa wajawazito
wanaweza kupata watoto wenye magonjwa ya moyo au mtindio
wa akili, kwa sababu chembechembe za ubongo hazikui vizuri.
Mara nyingi watoto huzaliwa na upungufu katika mwonekano
wa sura. Kwa mtoto pombe ni sumu kali, hata kama ni kwa kiasi
kidogo, itamdhuru.
Mama anaekunywa pombe anaweza kuwa hajali au kusahau
kujilinda mwili wake na mtoto anayekua.
Kama akipata maambukizo ya VVU na mtoto pia anaweza
akapata virusi vya UKIMWI.
Wanawake wanaovuta sigara wakiwa wajawazito wana
uwezekano mkubwa wa kuzaa watoto ambao hufariki ghafla bila
sababu ya kueleweka katika mwaka wao wa kwanza wa maisha.
Watoto wa akina mama wanaovuta sigara mara nyingi huzaliwa
na umbo dogo kuliko wengine kwa sababu watoto walipata
chakula kidogo walipokuwa bado tumboni mwa mama zao.
Ujumbe upo wazi: Wanawake wanaotaka watoto wenye afya
wasivute kabisa sigara wala kunywa pombe wakiwa wajawazito.
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_461e8c9950d3c5ad7218fca1a3e1847a, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Hapana, mbu na wadudu wengine hawawezi i kukuambukiza virusi vya UKIMWI kutokana na mfumo wa mii ...
Read More
Je, ni lazima kufanya ngono kwa sababu ya marafiki au shinikizo za kisiasa? 🤔
Ndugu vij...
Read More
Si kweli kabisa! Baada ya kuvuta bangi mtu hujiona kama jasiri sana na mwenye nguvu. Lakini madha...
Read More
Kila njia ya kuzuia mimba ina faida na hasara zake. Kwa mfano faida ya vidonge ni kwamba kama mwa...
Read More
-
Kujenga uhusiano wa kimapenzi wenye afya na mwenza wako ni muhimu sana. Hii ni kwa saba...
Read More
Habari za leo! Leo nataka kuzungumza juu ya jinsi ya kuonyesha ukarimu kwa msichana wako. Kama mw...
Read More
Je, katika kujaribu fantasia za ngono/kufanya mapenzi pamoja na mwenza wako? Hii ni mada ambayo i...
Read More
Hapana, huwezi kupona Virusi vya UKIMWI au UKIMWI kwa kufanya ngono na bikira. Hakuna tiba ya maa...
Read More
-
Anza kwa Kujijenga Kimaumbile
Kabla ya kumwomba msichana tarehe ya ushirikiano, ni muhi...
Read More
Bangi hupunguza mawazo kwa muda mfupi kwani huleta hisia za furaha na utulivu. Lakini hata hivyo ...
Read More
Kama mvulana, unajua kuwa mazungumzo na msichana yako yanaweza kuwa magumu sana. Unaweza kuwa na ...
Read More
Sababu mojawapo ni kuwa bangi hulimwa hapa nchini na
hivyo hupatikana kwa urahisi. Bangi huu...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!