Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e6d9fb0234ae0fdef54d44f211f043b1, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Faida 25 za kutembea kwa Miguu
Date: April 15, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanatumia vyombo mbalimbali vya usafiri kwenda karibu kila eneo.
Kwa hakika kutembea kwa miguu kuna manufaa mengi sana kwa ajili ya afya ya mwili, uchumi na maisha yako ya kijamii.
Ikiwa unapenda kuwa bora na mwenye tija zaidi katika nyanja zote, basi fahamu faida za kutembea kwa miguu.
- Hukabili maradhi ya moyo kwa kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu.
- Huimarisha mifupa.
- Huondoa au kupunguza hatari ya kupata kiharusi.
- Husaidia kupunguza uzito.
- Huzuia saratani ya utumbo mpana.
- Hukuwezesha kupata vitamini D kutoka kwenye jua.
- Hukusaidia kuboresha usawa wa mwili wako (balance).
- Hukabili maradhi ya kisukari. Unapotembea unafanya mazoezi yanayoleta uwiano wa urefu na uzito β BMI; jambo litakalokukinga na aina ya pili ya kisukari (Type 2 Diabets).
- Hukabili shinikizo la damu.
- Huondoa msongo wa mawazo.
- Huongeza utayari.
- Hukufanya ujifunze mambo mbalimbali kwa kuona.
- Hukuokolea gharama za nauli au mafuta.
- Hupunguza lehemu mbaya mwilini (cholesterol)
- Huimarisha misuli.
- Husaidia mmengβenyo wa chakula kwenda vizuri.
- Huwezesha kinga mwili kujiimarisha na kujijenga (kutokana na sababu kuwa kutembea ni aina ya zoezi).
- Huboresha uwezo wa kumbukumbu.
- Hukujengea mahusiano ya kijamii. Unapotembea utakutana na watu mbalimbali.
- Huzuia kuzeeka. Utafiti uliofanyika ulibaini kuwa watu wanaotembea umbali mrefu huishi zaidi.
- Hukuweka katika hali nzuri (mood).
- Hukusaidia kulala vizuri. Kumbuka mazoezi ni chanzo cha usingizi mzuri.
- Huboresha afya ya uzazi hasa kwa wanaume. Kutembea kama zoezi ni njia ya kuwapa wanaume nguvu katika afya ya uzazi.
- Huzuia kuharibika kwa mimba. Mazoezi ni muhimu sana kwa mama mjamzito kwa ajili ya afya yake na mtoto; hivyo zoezi rahisi na jepesi kwake ni kutembea.
- Huboresha mwonekano wa mwili. Mazoezi ni njia moja wapo ya kuufanya mwili wako uonekane katika umbo zuri. Hivyo kutembea kama aina mojawapo ya zoezi kunaweza kukusaidia sana.
Naamini umeona jinsi ambavyo kutembea kwa miguu kuna manufaa makubwa sana kwenye afya, uchumi na hata mahusiano yako ya kijamii.
Inashauriwa kuhakikisha unatembea kwa miguu angalau dakika 30 kila siku. Kwa njia hii utapata manufaa mengi yaliyotajwa hapo juu.
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_e6d9fb0234ae0fdef54d44f211f043b1, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Kuwa na harufu mbaya mdomoni ni kitendo kinachoweza kuathiri maisha ya mtu kimahusiano si kwa mpe...
Read More
Matunda yote yana faida mwilini kiafya lakini matunda yanatofautiana kifaida. Zifuatazo ni faida ...
Read More
Kitunguu swaumu hujulikana kama kitu cha kushangaza katika tiba huko mashariki ya mbali, Kitunguu...
Read More
Upungufu wa nguvu za kiume umekua tatizo kubwa sana kwa wanaume wengi. Tatizo hili limewakumba wanau...
Read More
Asilimia kubwa tunapenda kutumia karoti katika kuunga katika mboga ya nyama na si kuila karoti ka...
Read More
Mapera ni matunda yanayo patikana kwa wingi lakini mara nyingi huwa hayapendelewi sana kutokana n...
Read More
Kuna mambo ambayo huwa tunayachukulia ya kawaida na wala hatuko tayari kufahamu umuhimu wake. Jua...
Read More
NI muujiza! Pengine hivyo ndivyo yeyote anaweza kusema pindi akisikia kwa mara ya kwanza juu ya n...
Read More
Kukoroma ni tatizo linalowapata watu wengi wakati wanapolala ambalo linaweza kuwatokea watu wa kila ...
Read More
Watu wengi tumekuwa tukijali kazi zetu za kila siku bila kujali hali ya afya zetu matokeo yake ku...
Read More
JEE NYAMA YA NGURUWE (KITI MOTO) NI SALAMA KWA BINADAMU???
Hapa huwa kun...
Read More
Nimekutana na hiki kitabu japo nimekipitia juu juu nikaona nisiwe mchoyo Wa kukushirikisha wewe u...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!