Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_f986e240c4db2477fdd2581adb189dc8, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Faida 25 za kutembea kwa Miguu
Date: April 15, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kwa kiasi kikubwa. Hivi leo watu wanatumia vyombo mbalimbali vya usafiri kwenda karibu kila eneo.
Kwa hakika kutembea kwa miguu kuna manufaa mengi sana kwa ajili ya afya ya mwili, uchumi na maisha yako ya kijamii.
Ikiwa unapenda kuwa bora na mwenye tija zaidi katika nyanja zote, basi fahamu faida za kutembea kwa miguu.
- Hukabili maradhi ya moyo kwa kuhamasisha mzunguko mzuri wa damu.
- Huimarisha mifupa.
- Huondoa au kupunguza hatari ya kupata kiharusi.
- Husaidia kupunguza uzito.
- Huzuia saratani ya utumbo mpana.
- Hukuwezesha kupata vitamini D kutoka kwenye jua.
- Hukusaidia kuboresha usawa wa mwili wako (balance).
- Hukabili maradhi ya kisukari. Unapotembea unafanya mazoezi yanayoleta uwiano wa urefu na uzito β BMI; jambo litakalokukinga na aina ya pili ya kisukari (Type 2 Diabets).
- Hukabili shinikizo la damu.
- Huondoa msongo wa mawazo.
- Huongeza utayari.
- Hukufanya ujifunze mambo mbalimbali kwa kuona.
- Hukuokolea gharama za nauli au mafuta.
- Hupunguza lehemu mbaya mwilini (cholesterol)
- Huimarisha misuli.
- Husaidia mmengβenyo wa chakula kwenda vizuri.
- Huwezesha kinga mwili kujiimarisha na kujijenga (kutokana na sababu kuwa kutembea ni aina ya zoezi).
- Huboresha uwezo wa kumbukumbu.
- Hukujengea mahusiano ya kijamii. Unapotembea utakutana na watu mbalimbali.
- Huzuia kuzeeka. Utafiti uliofanyika ulibaini kuwa watu wanaotembea umbali mrefu huishi zaidi.
- Hukuweka katika hali nzuri (mood).
- Hukusaidia kulala vizuri. Kumbuka mazoezi ni chanzo cha usingizi mzuri.
- Huboresha afya ya uzazi hasa kwa wanaume. Kutembea kama zoezi ni njia ya kuwapa wanaume nguvu katika afya ya uzazi.
- Huzuia kuharibika kwa mimba. Mazoezi ni muhimu sana kwa mama mjamzito kwa ajili ya afya yake na mtoto; hivyo zoezi rahisi na jepesi kwake ni kutembea.
- Huboresha mwonekano wa mwili. Mazoezi ni njia moja wapo ya kuufanya mwili wako uonekane katika umbo zuri. Hivyo kutembea kama aina mojawapo ya zoezi kunaweza kukusaidia sana.
Naamini umeona jinsi ambavyo kutembea kwa miguu kuna manufaa makubwa sana kwenye afya, uchumi na hata mahusiano yako ya kijamii.
Inashauriwa kuhakikisha unatembea kwa miguu angalau dakika 30 kila siku. Kwa njia hii utapata manufaa mengi yaliyotajwa hapo juu.
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_f986e240c4db2477fdd2581adb189dc8, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Peasi ni tunda ambalo limekuwa halithaminiwi licha ya kuwa na faida lukuki katika mwili wa binada...
Read More
Asali hasa asali mbichi ya asili ni dawa nzuri sana ya kutibu chunusi. Asali ni antibiotiki ya as...
Read More
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinaz...
Read More
Leo tutaongelea mazoezi gani ya kawaida ambayo mama mjamzito anaweza kuendelea kuyafanya kila sik...
Read More
Matumizi ya maji ya kunywa ni moja ya dawa rahisi kabisa ya shinikizo la chini la damu.
Hii...
Read More
Ni msukumo wa damu ulio juu kuliko inavyotakiwa kwa muda mrefu. Msukumo wa damu huhitajika mwilini i...
Read More
Kwa ajili afya ya mama na mtoto ni muhimu sana, mwanamke anatakiwa apate chakula bora kilicho na ...
Read More
Kunywa Maji yenye chumvi husaidia kutibu shinikizo la chini la damu sababu sodiamu iliyomo kweny...
Read More
1.Usichelewe kwenda HAJA.Β Kutunza mkojo kweye kibofu chako kwa muda mrefu ni wazo ...
Read More
Tafiti zinasema kwamba mtu mmoja anayekunywa soda moja kwa siku, anakunywa zaidi ya galoni au dum...
Read More
Mshubiri au Aloe Vera kama ilivyozoeleka na namna nzuri kwa wale wote wanaotaka kubaki na ngozi ...
Read More
1.Kubana mkojo kwa muda mrefu
2.Kutokunywa maji ya kutosha kila siku
3.Kutumia chumvi n...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!