Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_f0edfc51bb7f6ce2ba3377c037139018, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Salamu za kuaga mwaka na kukaribisha mwaka mpya
Date: July 11, 2016
Author: SW - Melkisedeck Shine
KWAHERI MWAKA JANA. UMENIFUNZA MENGI.
Mwaka umefika mwisho, zimebaki siku tatu tu
kuingia mwaka mwingine lakini yapo mengi
niliyojifunza mwaka huu na pengine ningepesha
kushare:
1. Kwamba si lazima sana kuwa na rundo la
marafiki kama hawaleti positive effects kwenye
maisha yako. Urafiki wa maongezi yasiyoleta
maendeleo ni uzamani chakavu.
2. Matumizi madogomdogo yasiyo ya lazima
huchelewesha maendeleo makubwa yenye kiu na
mimi. Nmekuwa na matumizi yasiyo ya lazima na
ndio matundu hayo madogo yamezamisha meli.
3. Mungu ndio kila kitu. Anza na maliza siku na
Mungu. Ukikosacho hakukupangia, usiumie,
muombe akuletee atakacho.
4. Harusi zinaumiza. Usipojiwekea kiwango
maalum na idadi ya harusi za kuchangia kwa
mwaka na kwa umuhimu utakuja kujenga nyumba
kwenye harusi za wenzako.
5. Lawama ni muhimu sana ili maisha yaende,
usiogope hasa pale unapokuwa unasimamia lililo
la kimaendeleo kwako. Kumridhisha kila binadam
ni ngumu. Kuna muda ni kwa maendeleo yako
inabidi uwe mbinafsi.
6. Mapenzi ni mazuri ila yasikuzidi 'kimo', vipo
vyamaana vya kulilia sio mapenzi. Kikulizacho
ndicho ulichokipa kipaumbele. Mtu aamuapo
kukuliza na wewe ukalia basi umemtukuza.
Mapenzi yasiyosumbua na yaliyojaa mijadala ya
kimaendeleo ndiyo mapenzi yenye afya.
7. Watu waliowengi hasa kwenye mitandao ya
kijamii wana matatzo na ukichaa, usibishane nao
hasa kwenye mambo yasiyokuletea wewe
maendeleo. Usione hasara kuwafanya wajione
washindi.
8. Wazazi ni Muhimu sana, sala zao ni muhimu
kwako. Usipende kuhonga mpita njia akuachaye
siku yeyote ukawasahau wazazi wako. Wapo
watu sikukuu hizi wametumia maelfu ya shilingi
kuhudumia wanawake zao au wanaume zao
wapitaji wakasahau wazazi wao hata kwa pesa
ya dawa.
9. Kuahirisha mambo ni ugonjwa wa kuridhika na
dhiki. Uahirishapo atakaye uwe chini anafurahi.
Muaibishe shetani kwa mipango thabiti.
10. Panga kwaajili ya MWAKA kabla haUjafika,
kupanga kunakupa nafasi ya kujihakiki.
Mpya mwaka wa kucheza na 'altenatives'.
SEASON GREETINGSβ¦..HAPPY NEW YEAR.
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_f0edfc51bb7f6ce2ba3377c037139018, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
Watu wengi tunapenda sana Pesa lakini hatuko tayari kuzifanyia Pesa kazi nikiwa na maana kutumia ...
Read More
1. Epuka kugeuza mshahara wako kuwa mali ya ukoo. Kamwe mshahara wako siyo mali ya ukoo. Siku uta...
Read More
20 - 25 =Iwe kama ni kielimu hujafikia malengo yako,sitisha mara moja tafuta kazi/biashara ya kuf...
Read More
Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtu anayejengaΒ GHOROFAΒ na yule anayejengaΒ Read More
Kazi au shughuli unayoifanya ina thamani gani kwa wengine?unawasaidia au unawaumiza??
Biasha...
Read More
Ebu fikiria Dada anayechoma mahindi maeneo ya Manzese Darajani kuanzia saa 12 jioni mpaka SAA 2 u...
Read More
Siku hizi kuna tangazo moja la kampuni ya simu za mikononi, Tigo, likimuonesha mama akiwa _busy_ ...
Read More
Jifunze kanuni za fedha
kama ilivyoainishwa hapo chini.
Fedha inataki...
Read More
Bila shaka upo uhusiano mkubwa kati ya pesa na muda..
-Ndio maana nauli ya ndege ni kubwa k...
Read More
1. Hauko Tayari kuthubutu na kujiunga
2. Kutokujiamini
3. Kutopata sehemu sahihi ya kup...
Read More
Ukiona unalala masaa 9 wakati Donald Trump analala manne tu. Afu unaamka huna nauli na bado kesho...
Read More
Wengi wetu tunapenda Mafanikio, tunapenda kufika mbali tunapeda kuwa kama Mengi siku moja.
...
Read More
No comments yet. Be the first to share your thoughts!