Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_df4466c77e22a1b7d14a088c826c2c09, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/display_user.php on line
4
Mapishi ya Biriani
Date: April 9, 2022
Author: SW - Melkisedeck Shine
Mahitaji
Mchele (rice 1/2 kilo)
Nyama (beef 1/2 kilo)
Vitunguu (onion 2)
Kitunguu swaum (garlic 1 kijiko cha chai)
Tangawizi (ginger 1 kijiko cha chai)
Maziwa mgando (yogurt 1 kikombe cha chai)
Hiliki nzima (cardamon 6)
Amdalasini nzima (cinamon stick 2)
Karafuu nzima (cloves 6)
Pilipili mtama nzima (black pepper 8)
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Binzari manjano (turmaric 1/2 kijiko cha chai)
Binzari nyembamba nzima (cumin 1/4 kijiko cha chai)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia nyama na uikaange kwa muda wa dakika 10. baada ya hapo tia tangawizi, kitunguu swaum, hiliki(4), amdalasini (1), karafuu (4), pilipili mtama (5), Curry powder, binzari manjano, binzari nyembamba na chumvi. Kisha koroga. Baada ya hapo tia yogurt na uipike mpaka ikauke kisha tia maji kidogo, funika na upunguze moto na uache ichemke kwa muda wa nusu saa.Baada ya hapo nyama itakuwa imeiva na mchuzi kubakia kidogo.Kwahiyo itatakiwa kuiipua.
Loweka mchele kwa dakika 10. kisha chemsha maji mengi kidogo katika sufuria kubwa. baada ya hapo tia hiliki (2) amdalamsini (1) karafuu(2) pilipili mtama (3) chumvi na mafuta kiasi. acha ichemke kidogo kisha tia mchele.Hakikisha maji yameufunika mchele kabisa na uuache uchemke kwa muda wa dakika 8 tu (kwani hautakiwi kuiva kabisa) kisha uipue na uchuje maji yote katika chujio. baada ya hapo chukua sufuria ya kuokea (baking pot kama unayoiona kweye picha) Kisha weka wali nusu na uusambaze sawia kisha weka mchuzi nyama na mchuzi wake pia utandaze na umalizie kwa kuweka leya ya wali uliobakia. Baada ya hapo ufunike na uweke kwenye oven kwenye moto wa 200°C kwa muda wa nusu saa.na baada ya hapo biriani litakuwa tayari kwa kuliwa.
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_df4466c77e22a1b7d14a088c826c2c09, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in
/home/ackyshine/mhubiri/comments.php on line
4
Please log in or register to leave a comment or reply.
Related Posts
VIAMBAUPISHI
Mchele - 3 vikombe
Nyama ya kusaga - 1 LB
Mchanganyiko wa Nafaka...
Read More
Viamba upishi
Unga ngano vikombc 3
Unga mbegu za mchicha kikombe 1
Baking powde...
Read More
Vipimo
Wali:
Mchele mpunga - 4 Vikombe
Tui la nazi - 6 vikombe
Chumvi...
Read More
Mahitaji
Unga wa ngano ( self risen flour) kikombe 1 na 1/2
Hamira (yeast) 1 kijiko ...
Read More
Vipimo vya mseto
Tanbihi: Kiasi ya vipimo inategemea wingi wa watu, unaweza kupunguza au ...
Read More
Nini maana ya lishe?
• Lishe yahusu mafunzo ya chakula na jinsi miili ...
Read More
VIPIMO VYA WALI
Mchele wa hudhurungi (brown rice)
na (wild rice kidogo ukipenda)Osh...
Read More
Viambaupishi
Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2
Siagi 4 Vijiko vya supu
Maziwa (condensed...
Read More
Njia za kupima Afya
Njia mbalimbali hutumika kupima hali ya lishe, njia hizi ni;
Read More
Virutubishi
ni viini vilivyoko kwenye chakula ambavyo vinauwezesha mwili kufanya kazi zak...
Read More
Viamba upishi
Unga 2 Viwili
Sukari ya kusaga 1/4 Kikombe
Siagi 250 gms
...
Read More
Vipimo Vya Ugali:
Unga wa mahindi/sembe - 4
Maji - 6 takriban
No comments yet. Be the first to share your thoughts!